Faida Ya Biashara Ya Juice Ya Miwa Tanzania

Biashara ya kutengeneza juice ya miwa ina faida hivyo imekuwa maarufu sana katika mikoa mbalimbali hapa Tanzania. Hii inatokana na kinywaji cha juice ya miwa kuwa na faida nyingi katika mwili wa binadamu.

Faida ya juice ya miwa mwilini na kwenye biashara

  • Juice ya miwa inasaidia ni kusafisha mkojo, figo na kutibu homa ya manjano.
  • Juce ya miwa ni kiburudisho ambacho hukata Kiu hasa wakati wa joto.
  • Pia miwa ni jamii ya tunda lenye alkali hivyo lina uwezo wa kupambana na saratani hasa ile ya kibofu cha mkojo na saratani ya maziwa.
  • Sukari halisia ya miwa ni nzuri kwa mwili kwani ina virutubisho na madini kwa wingi.
  • Miwa ina faida nyingi kiafya Juice ya miwa inafahamika na wataalamu wa afya kwa kuwa na uwezo wa kuupa mwili nguvu kwa sababu ya glucose iliyopo. Kijiko kimoja cha juisi ya miwa kina kalori 11.
  • Madini halisi na vitamin zinazopatikana katika sukari ni kama phosphorus, calcium, madini ya chuma na potassium.
  • Miwa ina upekee wake kwani ina uwezo wa kuongeza maji mwilini, inaupooza mwili na kuupa nguvu.
  • Biashara ya juisi ya miwa ni moja kati ya biashara ndogo inayoweza kuanza na mtaji mdogo lakini ikakuletea faida kubwa kama mjasiriamali kulingana na uhitaji wake.

Mambo ya kuzingatia wakati wa kuanzisha biashara ya juice ya miwa

  1. Mashine ya kukamua miwa – TZS 300,000 – 400,000
  2. Glasi nzuri za ujazo tofauti – TZS 20,000
  3. Chujio – TZS 5,000
  4. Beseni – TZS 8,000
  5. Ndoo 2 – TZS 5,000
  6. Jaba kubwa la uchafu – TZS 12,000
  7. Mtaji wa kununua miwa –TZS 50,000
  8. Tolori la kusafirisha – TZS 60,000
  9. Vifaa vingine – TZS 40,000

Jumla ya mtaji wa kuanzisha biashara ya juice ya miwa ni TZS 640,000

Muwa mmoja unaweza ukatengeneza lita 4 za juisi na muwa mmoja unaweza ukaununua kwa TZS 300 kwa bei ya jumla. Lita moja ya juice ya miwa utauza kwa bei ya TZS 1,000 hivyo kwa muwa mmoja unatengeneza TZS 4,000

Mjasiriamali anaweza akaongeza ubunifu kwa kuongeza tangawizi au limao katika juisi yake ya miwa ili kuongeza ladha. Biashara hii ni nzuri hasa inapofanyika sehemu yenye mzunguko wa watu wengi kama stendi ya mabasi, na kwenye masoko

Changamoto za biashara ya juice ya miwa

  1. Changamoto zinazo wakabili wauzaji wa juice ya miwa ni upatikaji wa bidhaa hiyo kwa msimu
  2. Baadhi ya watu kutoamini maji wanayotumia wauzaji katika kutengenezea juisi kama ni salama kwa afya zao.
  3. Serikali imepiga marufuku vinywaji visivyo pimwa na TBS hivyo wakati mwingine ni usumbufu kwa mjasiriamali mdogo wa biashara ya juisi ya miwa.
  4. Wajasiliamali wa biashara hii wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu wa mazingira bora ya kufanyia kazi zao Mfano uwepo wa wadudu kama nzi na nyuki mahali zinapofanyika biashara ya uuzaji wa juice ya miwa.
Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

16 Comments
  1. Asante kwa Elimu Hii ya Ujasiriamali Pia Nimefurahi sana kupata taarifa kuhusu biashara ya juisi ya miwa.

  2. Asante kwa elimu hii ya biashara ya juice ya miwa hivi karibuni nitaanza kujifunza jinsi ya kukamua miwa.

  3. Nimefurahi kuona Hii post yako Asante sana na Pia na naomba uzidi kutujulisha faida za biashara mbalimbali.

  4. Nimependa na Nimejifunza Vizuri Biashara ya Juice Miwa Bado Najipanga ipo Siku Najua Nitaanza Kuifanya.

  5. Habari biashara ya juice ya miwa naipenda kweli.

  6. Tatizo kwangu ni mashine za kukamua juice hapa najichanga siku ikifika tu naanza hii biashara.

  7. Nashukuru sana kwa kupata elimu nzuri ya biashara ya uuzaji wa juice ya miwa

  8. Siku yoyote nikinunua tu mashine ya juice ya miwa basi nitaanza biashara siku hiyo hiyo.

Leave a reply